Simon Ockley
Simon Ockley
(1678-1720) Profesa wa lugha ya kiarabu katika chuo kikuu Cambridge:
¡°Jambo moja maalum ambalo lapaswa kugunduliwa kwa Ali, ni kwamba
mama yake alimzaa Makka ndani ya Al-Kaaba, ambapo haijawahi kutokea
kwa mtu yeyote.¡±
Namna hii anakubainishieni Mwenyezi Mungu Aya zake ili
mpate kufahamu
(Qur'an 2:242)
[History of the Saracens, London, 1894, Uk. 331]
Washington Irving
(1783-1859) Aalijulikana kama ¡°The first American man of letters¡±:
"Ali alikuwa anatokana na tawi lenye heshima kuu katika matawi ya
kikureishi. Alikuwa na sifa tatu zilizokuwa zikitukuzwa sana kwa waarabu:
Ujasiri, ufasaha na ukarimu. Moyo wake usio na hofu ulimpatia sifa kutoka
kwa Mtume ya kuwa simba wa Mungu, mifano ya ufasaha wake imebaki
katika baadhi ya semi na kuhifadhiwa miongoni mwa waarabu; na ukarimu
wake ulionekana dhahiri katika kupenda kwake kugawanya na watu, kila
siku ya ijumaa, kile kilichobaki katika hazina. Kuhusu utukufu wake,
tumetoa mifano mara kwa mara; utukufu wake ulichukia kila kitu chenye
udanganyifu na uchoyo."
Wasiokuwa Waislamu wanasema
nini juu ya ¡
[Lives of the Successors of Mahomet, London, 1850, Uk. 165]
"Yeye alikuwa ni mmoja wa miongoni mwa wa mwisho na wenye thamani
miongoni mwa waislamu wa kale, ambaye alikusanya nguvu ya kidini kwa
ushindi akiwa na Mtume mwenyewe, na kufuata ruwaza ya mwisho kabisa
ya Mtume Muhammad. Yeye ni mtu anayetajwa kwa heshima kama khalifa
wa kwanza aliye kirimu na kulinda elimu. Alikuwa ndani ya mashairi yeye
mwenyewe, na nyingi miongoni mwa methali na semi zake zimehifadhiwa
na kufasiriwa katika lugha mbalimbali. Pete lake ulikuwa na maandishi hili:
'Ufalme ni wa Mwenyezi Mungu'. Moja katika semi zake inaonyesha jinsi
alivyokuwa hathamini vivutio vinavyopita tu vya dunia, ni (kusema kwake):
'Maisha ni kivuli tu cha mawingu - ndoto ya mwenye kulala.'"
'Ali
MRITHI WA KWANZA WA
MTUME MUHAMMAD
(Rehma na amani ziwe juu yao)
[Lives of the Successors of Mahomet, London, 1850, Uk. 187-8]
Robert Durey Osborn
(1835-1889) Meja wa kikosi cha the Bengal Staff Corps:
¡°Pamoja naye umepotea moyo hasa na Muislamu bora ambaye Historia ya
Mohammad imehifadhi kumbukumbu hiyo.¡±
[Islam Under the Arabs, 1876, Uk. 120]
kwaw kujua habari zaidi juu ya Imam 'Ali bin Abi Talib, tazama Tovuti:
v1.0
Imam Ali bin Abi Talib alikuwa ni mrithi wa Mtume
Muhammad, amani ziwe juu yao. Huu ni mkusanyiko wa
nukuu fupi fupi kumhusu yeye kutoka kwenye maelezo mbali
mbali ya wasomi wa imani nyingine, wakiwamo wanataaluma,
waandishi, wanafalsafa, washairi, wanasiasa na wanaharakati.
Thomas Carlyle
Dr. Henry Stubbe
(1795-1881) Mwanahistoria mskochi, mkosoaji, na mwandishi wa elimu ya jamii:
(1632-1676) Muhafidhina, Mwanafizikia, na mwanafalsafa:
¡°Kuhusu huyu kijana Ali, mtu yeyote atampenda tu. Ni kiumbe mwenye
akili kuu, kama anavyojionyesha yeye mwenyewe sasa, na kila siku na
baadaye; mwenye mapenzi maridhawa, mwenye ujasiri wa hali ya juu. Ana
uungwana; shujaa kama simba; huku akiwa na huruma, ukweli na mapenzi
yafaayo kwa imani ya kikristo.¡±
[On Heroes, Hero-Worship, And the Heroic in History, 1841, Hotuba 2: The Hero
as Prophet. Mahomet: Islam., Mei 8, 1840)]
¡°Hakuipenda dunia na mapambo yake bali alimcha sana Mwenyezi Mungu,
alitoa sadaka nyingi, alikuwa mwadilifu katika vitendo vyake vyote,
mnyenyekevu na mwepesi wa kuzoeana na watu; huku akiwa na maneno ya
ya haraka ya kufurahisha na ubunifu usio wa kawaida, alikuwa na elimu
maridhawa, sio elimu zinazoishia kwa maneno tu bali zinazoendelea kwa
vitendo.¡±
[An Account of the Rise and Progress of Mahometanism, 1705, Uk. 83]
Edward Gibbon
Gerald de Gaury
(1737-1794) Mwanahistoria mkuu wa kiingereza katika enzi zake:
(1897 - 1984) Mwanajeshi mahiri na mwanadiplomasia:
"Sifa kuu alizokuwa nazo Ali hazikuzidiwa na mbadilishaji dini yeyote wa
siku za hivi karibuni. Alichanganya sifa za kuwa ni mshairi, mwanajeshi, na
mcha Mungu; busara zake bado zinapatikana kwenye mkusanyiko wa
misemo yake ya kimaadili na ya kidini; na kila adui, kwenye vita vya
maneno au vya upanga, alishindwa na ufasaha na ujasiri wake. Kuanzia saa
ya mwanzo ya ujumbe wake wa dini mpaka mwisho wa ibada za kuzikwa
kwake, Mtume Muhammad hajaachwa kuwa na rafiki mkarimu, ambaye
alifurahishwa kwa kumwita kuwa ni ndugu yake, wasii wake, na kuwa yeye
(Ali) ni ¡®Harun mwaminifu¡¯ wa ¡®Nabii Musa¡¯ wa pili."
[Rulers of Mecca, London, 1951, Uk. 49]
Wilferd Madelung
Profesa wa lugha ya kiarabu, chuo kikuu cha Oxford:
[The Decline and Fall of the Roman Empire, London, 1911, Juz. 5, Uk. 381-2]
Philip Khuri Hitti
(1886-1978) Profesa wa lugha za kisemiti, Chuo kikuu cha Princeton:
¡°Shujaa vitani, mwenye busara katika ushauri, fasaha wa kuzungumza,
mkweli kwa marafiki zake, anayeheshimiwa na maadui zake. Yeye alikuwa
ni ruwaza wa heshima na maadili mema ya kiislamu. Na alikuwa ni
Suleiman wa utamaduni wa kiarabu, ambapo kwake mashairi, methali,
hotuba na simulizi - zisizo na idadi - zimekusanyika.¡±
[History of the Arabs, London, 1964, Uk. 183]
Sir William Muir
(1819 - 1905) Msomi na kiongozi wa kiskochi. Alikuwa na wadhifa wa Waziri wa
mambo ya nchi za nje katika serikali ya India, pia alikuwa Lieutenant Gavana wa mkoa
wa Kaskazini Magharib:
¡°Alijaaliwa kipaji cha maarifa, mwenye mapenzi, na mwenye kujifunga na
urafiki, tangu uvulana wake alikuwa amejitolea roho na moyo wake kwa
Mtume. Mnyenyekevu, mpole, na asiyependa makuu. Ambapo baada ya
kupita siku kadhaa, alipotawala nusu ya ulimwengu wa kiislamu, kwa
hakika alilazimishwa pasi na kutaka.¡±
[The Life of Mahomet, London, 1877, Uk. 250]
¡°Alikuwa ana hekima sana katika kutoa ushauri, na shujaa vitani, mkweli
kwa marafiki zake na mkarimu kwa maadui zake. Yeye daima alikuwa ni
ruwaza ya heshima na maadili mema ya kiislamu.¡±
"Kwenye madai ya uongo ya Bani Umayya ya kuuhaalisha utawala wa
Mwenyezi Mungu kuwa wao ni makhalifa wa Mungu duniani, na ulaghai
wao na serikali yao yenye mizozo na kulipiza kisasi, pamoja na hayo yote,
waliukubali uaminifu wake kutolegalega kwake na kujitolea katika
kuutumikia uongozi wa kipindi hicho wa kiislamu, uaminifu wake binafsi,
kuwatendea usawa wote waliomuunga mkono na pia ukarimu wake wa
kuwasamehe maadui wake aliowashinda."
[The succession to Muhammad: a study of the early caliphate, Cambridge, 1997,
Uk. 309-310]
Charles Mills
(1788 - 1826) Mwanahistoria bingwa wa enzi zake:
¡°Akiwa ni kiongoazi wa familia ya Hashim na binamu na mkwe wa
(Mtume) ambaye waarabu walimheshimu¡ inashangaza kuwa Ali
hakuandaliwa kuwa khalifa mara tu bada ya kufa Muhammad. Pamoja na
heshima ya kuzaliwa kwake na ndoa yake, pia alikuwa na urafiki na Mtume.
Huyu mtoto wa Abu Talib alikuwa ni wa mwanzo kuingia Uislam na
alikuwa ni kipenzi cha Mohammad, kwani alikuwa ni wa pili kama
alivyokuwa Harun kwa Musa. Kipaji chake kama msemaji, na ujasiri wake
kama shujaa, vilitukuzwa na taifa ambalo ujasiri ulikuwa ni sifa njema na
ufasaha ulikuwa ni busara.¡±
[An history of Muhammedanism, London, 1818, Uk. 89]
................
................
In order to avoid copyright disputes, this page is only a partial summary.
To fulfill the demand for quickly locating and searching documents.
It is intelligent file search solution for home and business.
Related download
- kwanini muislamu haruhusiwi kusherehekea maulidi
- mtume muhammad s a w katika biblia
- abu huraira sahaba wa mtume
- mfano mwema wa mtume muhammad s a w
- risala fupi ya kumuwezesha mtu kupambanua ni ipi dini ya haki swalehe
- بسم الله الرØمن الرØيم
- shaykh al islam ibn taymiyya mwana chuoni wa wana chuoni
- sherh ya misingi mitatu
- most nb dec swahili
- kuzaliwa kwa yesu kristo
Related searches
- notes to inspire simon sinek
- what s your why simon sinek
- who is simon sinek
- simon sinek ted talk why
- simon sinek better together quotes
- leadership quotes simon sinek
- simon sinek find your why worksheet
- simon sinek official website
- simon sinek quotes to inspire
- simon sinek quotes about leadership
- simon sinek quotes teamwork
- what is simon sinek s why