JunI 16, 2005 Gaudensia:Aishi kwa kuponda mawe
"Kutunza yatima ni jukumu letu wote"
JunI 16, 2005
Gaudensia:Aishi kwa
kuponda mawe
NA JOSEPH KITHAMA
Akiwa na umri wa miaka minne na nusu na mtu wa kuvutia, Bi Gaudensia Chuki alitarajia kufaidi upendo wa wazazi haki ya kucheza michezo ya kitoto na haki yake ya kimsingi ya elimu, inayotambulika kimaitaifa.
Hata hivyo, mtindo wa maisha wa Gaudensia, mkazi wa Isamilo katika Wilaya ya Nyamagana, ni ukanusho wa kweli wa haki zote za msingi zinazofurahiwa na watoto wa rika lake kila mahali duniani.
Mikono yake nyororo haijapata kumgusa mwanaserere au mchezo wa kompyuta kwa ajili ya watoto na badala yake, wakati wa umri mchanga wa miaka mitatu, Unaiwe Perusi Yusufu (56) alimpa Gaudensia nyundo ndogo ya kuvunjia mawe.
"Alianza kuvunja mawe kwa ile nyundo ndogo lakini hivi sasa anatumia nyundo kubwa zaidi, amezoea," bibi yake, anayeongoza familia ya watoto watatu waliotelekezwa; na mama yake aliye mgonjwa, alisema.
Kwa Gaudensia kuvunja mawe ndio uhakikisho pekee wa maisha. Hakuchukulii kama mfanyishaji kazi watoto, ambako kumeharamishwa na Shirika la Kimataifa la Kazi (ILO), lakini kama njia ya kujikimu kwa kijungu jiko.
Gaudensia huvunja mawe kiasi cha kutosha kujaza mawe galoni mbili zilizokatwa sawa kila siku, pamoja na kaka zake wakubwa na bibi yao ambaye lazima avunje mawe kujaza ndoo kumi na mbili katika vita vya kuwafanya watoto waliotelekezwa waishi katika nyumba ya matope kwenye miteremko ya milima ya Isamilo.
Familia hiyo yatima ambayo inaishi katika matatizo yaliyokithiri inabidi ivunje mawe kila siku kujaza lori na kuuzwa kwa Tsh. 30,000. "Kwa kawaida, tunauza ndoo za mawe yaliyovunjwa kwa kati ya Tsh. 200 na Tsh. 400, ili walau tupate pesa chache za kununulia unga na dagaa,"
Gaudensia alisema. Baba alimtelekeza Renatus Tito
(13), Lucas Peter (10) na Gandensia miaka kadhaa iliyopita kwa sababu alizozijua mwenyewe. "Baadhi ya watu wanasema hivi sasa anaishi Dar es Salaam. Nani anajua! Wala hatuelewi aliko.
Familia hiyo haina chanzo chochote kingine cha kipato ila kuvunja mawe. Ni kaya isiyo na ardhi inayoongozwa na bibi asiye na uwezo wa kifedha, wa kukodi sehemu ya kulima, ambayo inagharimu Tsh. 30,000 kwa nusu ekari.
Soko la mawe yaliyovunjwa halina uhakika siku zote. Kunapokuwa na kazi ya ujenzi, familia inahakikishiwa mahali pa kuuzia mawe yaliyovunjwa, kama ilivyo hivi sasa Isimalo ambako inatengenezwa barabara ya changarawe.
"Katika nyakati kadhaa, tunashuka hadi Tsh. 200 kwa ndoo ya mawe yaliyovunjwa kutokana na ukosefu wa soko la kutegemewa Isamilo, Kata ya pekee ya Mwanza, yenye mchanganyiko wa watu wakwasi na wale wanaoishi katika mazingira magumu sana, lakini ambao wanaelekea kujali kidogo kuhusu tabaka linaloishi katika hali ngumu.
Familia hiyo haiwezi kumudu gharama za matibabu ila vidonge vya panadol, ambavyo ni vya kupunguza maumivu tu. "Tunamwomba Mungu kwa dhati atunusuru tusiugue," bibi alisema, akifunga mikono yake kwa kukata tamaa.
Karibu tu, kuna bibi mwingine, Bi Sawata Maye (50), ambaye peke yake, anawalea watoto saba wanaotoka kwenye familia mbalimbali zinazohusiana naye.
Katika hawa watoto wenye umri wa kati ya miaka miwili na 13, watoto watatu walishindwa hata kujiandikisha elimu ya bure inayotolewa na MEMKI kwa vile wao ni maskini mno kumudu kununua hata sketi ya Tsh. 2000.
Wenzi wao watatu tofauti ambao ama walikufa kwa UKIMWI au waliwatelekeza tu watoto wao kwenye
Gaudensia Chuki akiponda mawe, kama njia pekee ya kuishi
nyumba ya bibi kuchota maji kujaza kati ya mapipa mawili au matatu kila siku ili kupata Tsh. 3,500 ili kuhakikisha kwamba watoto wanaishi katika hali ya uzoefu wanaokabiliana nao.
Ingawa mvua zinazoendelea ni ishara njema kwa watu wengi, lakini kwa Sawata, ambaye kuishi kwake kunategemea uuzaji maji, mvua hizo zinayatishia maisha ya watoto wake wanaoishi katika mazingira ya hatari.
Mtoto huyu ameweza kuhudhuria shule baada ya kupewa suruali ya mtumba na Msamaria Mwema, alisema bibi ambaye huyalisha matumbo ya watoto wote waliomzunguka kwa kuuza maji kutoka kwenye bomba lililofungwa na mkazi wa Isamilo mwenye hali nzuri.
Bi Christine Mashiku, Afisa Mtendaji wa Kata ya Isamilo, anasema
watu wenye hali nzuri Mwanza
wanaishi Isamilo, eneo lililojitenga
ambalo linaweza kufananishwa na
Oysterbay, Dar es salaam. Lakini Kata
hiyo pia ni makazi ya watoto 500
wanaoishi katika mazingira ya hatari
sana (MVC), chini ya umri wa miaka
18, kwa mujibu wa utafiti wa MVC
uliofanywa Januari 2005.
Kata ya Mwanza ina watoto
wanaoishi maisha ya hatari sana ina
asilimia 6.3 ya karibu watoto 15,000
walio chini ya umri wa miaka 18
iliyozungukwa na mawe.
Changamoto
zilizobainishwa
ambazo watoto wanaoishi katika
mazingira magumu, wanakabiliana nazo
Isamilo ni pamoja na vitu vya msingi:
chakula, malazi, ukosefu wa elimu,
ukosefu wa upendo, magonjwa sugu na
kujihusisha na uhalifu.
Utafiti wa Benki ya Dunia wa hivi karibuni katika Tanzania, Uganda na Zambia umegundua kwamba mababu na mabibi walifanyiza aina moja pekee kubwa kabisa inayowatunza yatima. Wazee wanauza ardhi, mali, wakiwemo ng'ombe na mali nyinginezo katika harakati za kupata mahitaji yao wenyewe yaliyo muhimu, na kuwatunzia wajukuu wao.
Tarakimu za hivi sasa duniani zinakadiria kwamba watoto milioni 16 walio chini ya umri wa miaka 15 wanapoteza ama mmoja wa wazazi au wazazi wote wawili kutokana na UKIMWI, na watoto milioni 40 wengine watawapoteza wazazi wao katika miaka 10 mingine ijayo.
Mtoto anahangaika kutunza wadogo
Katarina Mayala, akiwa karibu kutoa machozi wakati akielezea namna mama yao alivyo watelekeza huko Kirumba Mwanza. Nyuma ni kibanda walichoa azimwa na masamaria mwema
Kibanda cha matofali ya udongo, kisicho na madirisha na kuezekwa mabati yaliyoshikizwa kwa mawe yaliyosambaa paani kipo Mwanza karibu na kaburi la marehemu baba wa watoto watatu waliotelekezwa na mama yao.
Yawezekana marehemu baba huyo akawa amepumzika kwa amani katika makaburi ya familia yaliyopo jirani, lakini maskini watoto hao watatu wanahangaikia maisha yao ndani ya kibanda hicho walichopewa msaada na msamaria mwema bada ya kubomoka kabisa kwa kile cha kwanza, kilichokuwa cha bibi yao ambaye pia ametangulia mbele ya haki.
Miaka mitatu tu baada ya kifo cha baba yao mpendwa, Katarina Baliba (17), Mayala Baliba (13) na Emmanuel Baliba (11) walitupwa Kibuhoro katika Kata ya Kirumba na mama yao aliyekimbilia Nyegezi kuolewa na mume mwingine.
Mara chache sana huwatembelea watoto wake akiwa mikono mitupu, na kuwaacha kama walivyo bila hata ya dalili ya huruma, majirani wa watoto hao walieleza mbele ya Katarina aliyekuwa akibubujikwa na
machozi. Katarina alilazimika kubeba jukumu la
kuongoza familia ya watoto watatu tangu alipokuwa na umri wa miaka 14, bila ya msaada wowote wa fedha za kuendeshea maisha yake na ndugu zake wawili wa kiume.
Kumbukumbu ya majuto na uchungu mama huyo aliyomwachia Katarina ameshindwa kabisa kuivumilia. "Kila tunapomtembelea Katarina, anatutia uchungu na kutufanya tulie' alisema kwa kuomboleza Bi. Iluminata Mwita, Ofisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi wa Mwanza, wakati Rose Ahmed, Mwanamke mwingine aliyetusindikiza kwa watoto waliotelekezwa alikuwa akitokwa na machozi.
Katarina hakwenda shule yoyote ya msingi kwa sababu alichukua majukumu yote ya mama yake. Wakati fulani alilazimika kuwaachia ndugu zake kitanda na akalala chini, ambako kulikuwa kumelowa na mvua.
"Wakati mwingine tunalazimika
kukihama kibanda chetu usiku wa manane
ili kuokoa maisha yetu kutokana na mabati yaliyoshikizwa ambayo yanaweza kuzolewa na kimbunga au kuvuja wakati wa mvua," alisema Katarina, huku akilia kwa uchungu.
Kama vile kisa kisicho mwisho cha mateso ya moyo waliyonayo watoto waliojikuta kuwa wametelekezwa hakitoshi, Katarina alilazimika kuacha masomo katika shule ya Ufundi stadi mjini Mwanza alikotaka kusomea kuunga vyuma, kutokana na kuumwa.
Watu wenye moyo wa upendo wa Mwanza wanatafuta uwezekano wa kumfadhili Katarina akachukue masomo ya ufundi Cherehani yatakayomfaa kutokana na afya yake. Idara ya Maendeleo ya Jamii inaratibu michango ya kumsaidia binti huyo.
Kusema kweli maisha ya watoto hao watatu yanategemea msaada wa chakula wanaopewa na taasisi ya kikatoliki, iitwayo SHARON. Shirika hilo la misaada ndiyo dhamana pekee ya maisha yao.
Siku ya Mtoto Wa Afrika imekuwa ikisherehekewa tokea mwaka 1991, kwa madhumuni ya kuleta mwamko katika jamii kuhusu mambo yenye athari kwa watoto. Nchini Tanzania maadhimisho ya siku hiyo yamekuwa yakiwajumuisha watoto. Ujumbe wa mwaka huu: "Kutunza yatima ni jukumu letu wote"
2
Mahojiano na Mwakilishi wa UNICEF Tanzania
Bw. Rodney Phillips, kuhusu hali ya yatima nchini
SWALI:
Mababu
na
mabibi, ambao ndilo kundi moja
kubwa la watu wanaolea yatima
nchini Tanzania wanawezaje
kusaidiwa?
JIBU: Tatizo la VVU/UKIMWI
karibu limemaliza kizazi kizima cha
wazazi na walezi wa watoto. Hivi sasa
tunawaona mababu na mabibi ambao nao
pia ni wagonjwa wakiwalea wajukuu zao.
Kaya zinazoongozwa na mabibi na
watoto wengine, ziko katika hatari
kubwa sana. Hivyo, walezi wa yatima na
walio katika hali ya hatari sana wanahitaji
msaada wa haraka. Ukubwa wa tatizo
lenyewe unahitaji mtazamo wa kijamii.
Jamii hazina budi zijihamasishe na
kujipanga zenyewe kuona jinsi
wanavyowasaidia yatima na watoto
wengine walio katika mazingira
magumu. UNICEF husaidia ubainishaji
wa watoto walio katika mazingira ya
hatari kabisa katika jamii kadhaa kwa
kuhamishia taslimu na vifaa moja kwa
moja kwenye jamii hizo.
SWALI:
UNICEF
inaisaidiaje Tanzania kukabiliana na
tatizo la zaidi ya yatima milioni
mbili?
JIBU: Kimsingi jukumu la kuwalea
yatima ni la uongozi wa serikali
ikisaidiana na Vyama vya Kiraia na
Mashirika ya Kijamii. Wizara ya Kazi,
Maendeleo ya Vijana na Michezo
imeanzisha mpango bora kabisa wa
utekelezaji wa jinsi ya kuwasaidia yatima
nchini. UNICEF itakuwa ikisaidia
utekelezaji wa mpango huu wa
utekelezaji, na uhamasishaji wa rasilimali
zitakazohitajika.
SWALI:
Je, Malengo ya
Maendeleo ya Mileniam kuhusu
Watoto yanatekelezeka Tanzania
ambako VVU/UKIMWI huua watu
wengi?
JIBU: VVU/UKIMWI wenyewe ni
lengo la milenia, lengo Na. 6 ?
lililopangwa kidunia kwa kila nchi.
Tanzania inapaswa ipange malengo yake
halisi, ambayo si lazima yawe ndani ya
muda wa malengo ya dunia. Malengo ya
hivi karibuni lazima yaakisi rasilimali
zilizomo nchini, na kuhusisha miaka
mitatu hadi minne ijayo. Hili litasaidia
maendeleo ya viashiria vya ufuatiliaji
vilivyo sahihi zaidi, na uwajibikaji
mkubwa zaidi wa kisiasa.
SWALI:
UNICEF
inaisaidia serikali ya Tanzania katika
kuwalinda watoto dhidi ya
unyanyasaji, unyonyaji na nguvu?
JIBU: Hilo ni eneo nyeti! Si
kwamba ni afya na elimu ya watoto tu
ndiyo muhimu, bali hata uelewa wa
kitaifa wa vitendo dhidi ya unyonyaji,
utekelezaji, matumizi ya nguvu na
unyanyasaji wa watoto. Uelewa
utawawezesha watoto kuzijua haki zao.
Mifumo ya kisera na kisheria
inayoshughulikia uvunjaji wa haki za
mtoto haina budi kuharakishwa na
kutekelezwa. UNICEF inaisaidia serikali
katika uendelezaji.
Sheria ya Watoto, ambayo itaimarisha
ulinzi wa watoto, balehe, na vijana
SWALI:
Ni njia ipi iliyo
bora kuwashughulikia yatima
Tanzania ? kuishi na ndugu au
katika nyumba za yatima?
JIBU: UNICEF haiungi mkono
nyumba za yatima kama njia ya kwanza
ya kutatua tatizo. Ni vema kwa yatima
kuishi na ndugu zao, katika jamii.
Tunajaribu kuwasaidia kupitia walezi wao
katika kaya za jamii. Nyumba za yatima
zenyewe zaweza kuwa chanzo cha
matumizi mabaya ya mtoto.
SWALI:
Matarjio
ya
muda wa kusihi yanapungua, hasa
kutokana na HIV/UKIMWI. Je,
Tanzania ina uwezekano wa
kubadili hali hiyo kupitia
uboreshaji wa lishe na
huduma za afya?
JIBU: Ndio, lishe na afya ni
muhimu katika kuongeza
matarajio ya muda wa kuishi,
lakini pia elimu, ambayo ni
chanjo ya kijamii dhidi ya
VVU/UKIMWI. Tanzania ina
utashi wa kisiasa wa kuongeza
matarajio ya muda wa kuishi
kwa watu wake, ikitumia
rasiliamli zake. Iwapo serikali,
vyama vya kiraia na Asasi zisizo
za Kiserikali zikifanya kazi kwa
karibu, wanaweza kupata njia ya
kubadili hali ya kushuka kwa
matarajio ya muda wa kuishi.
Mpango wa sasa wa kuongeza
uchumi na kupunguza umaskini
? MKUKUTA ? unatupa
misingi ya kuwa na matumaini
si UNICEF tu bali mfumo wa
UN kwa ujumla unaunga
mkono malengo na mikakati ya MKUKUTA, katika kupanua Mwakilishi wa UNICEF Tanzania Mr Rodney
ubia kwa watoto.
Phillips akifurahi na watoto
Kwa nini Watanzania wanapendelea kutoa michango
mikubwa ya arusi kuliko kusaidia elimu ya watoto?
Yafuatayo hapa chini ni madondoo ya
watu wa aina mbalimbali kutoka Dar es
salaam na Zanzibar.
Bwana Barabona Thomas Morongo,
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la
Watu
Wanaopambana
na
VVU/UKIMWI
(WAMATA),
anakumbuka jinsi arusi aliyohudhuria
hivi karibuni ilivyotumia mamilioni ya
shilingi zilizochangwa na watu
wachache wenye uwezo, Dar es salaam.
Sherehe ya arusi hiyo ilikuwa na
orodha ya vyakula vya ziada, kama vile
uji, maziwa na vingine, ambavyo
baadhi yake wageni hata hawakuvionja.
Bwana Morongo anasema kwamba
baadhi ya watu waliochangia zaidi ya
shilingi milioni moja wakati wa
maandalizi ya arusi hiyo wana ndugu
na yatima wanaoishi katika hali mbaya,
pembeni mwao.
Bw. Morongo anadhani kwamba
msimamo wa kuchangia arusi za
kifahari badala ya kuwasaidia watoto
wanaoishi katika mazingira magumu
unatokana na urithi wa ujamaa wa
kiafrika.
"Ujamaa ulipandikiza katika vichwa
vya watu mawazo mabaya kwamba
watoto ni mali ya serikali. Kwa hiyo,
serikali ndio asasi ya pekee
inayotarajiwa kuwahudumia."
Anatoa mfano wa mikoa ya Kagera
na Kilimanjaro, ambayo haikuathiriwa
na urithi wa ujamaa kwa kiwango
kikubwa, akizingatia kwamba katika
mikoa hiyo watu wengi walifanikiwa
kuwapeleka watoto wao shule,
wakitumia pesa zilizochangwa na jamii.
Dkt.Mushy Conrad anasema
kwamba watu walio wengi
wanachangia zaidi kwenye arusi kuliko
ustawi wa yatima kwa ajili ya fahari
kuu wanayoipata wanapoahidi kiasi
kikubwa cha fedha mbele ya wenzao.
"Wanadhani kuwachangia yatima ni
mpango wa muda mrefu ambao hauna
budi ushughulikiwe na serikali.
Conrad anasema, kwa kweli
waunda sera wengi na baadhi ya
wanajamii wasiowajibika walipata
elimu yao bure. "Iwapo wao
walisaidiwa kwa nini wasiwasaidie
wengine? "Conrad anauliza.
Rose Muthamia, 20 mkazi wa
Mwanayamala anahusisha na tabia ya
kujionyesha, wahusika wakitaka kila
mtu azingatie uwezo wao. Shauku
nyingine ambayo Muthamia anaitoa ni
ile ya kuamini kwamba yatima ni
wajibu wa ndugu wa yatima hao,
wakisahau kwamba baadhi ya ndugu
wa yatima ni maskini wa kutupwa.
Kula, kunywa na kufanya sherehe ni
shughuli za kijamii zinazopendwa na
Watanzania walio wengi anasema John
Mujulizi 34, mfanyabiashara wa Jiji, na
kwamba wachangiaji wa starehe za
arusi wanasimuliwa na hujifurahisha
kwenye starehe ya arusi.
Anasema kwamba kwao michango
ya sherehe za arusi hatimaye hutumika
kwenye tafrija ikilinganishwa na
vitendo vya kumsaidia yatima ambaye kutoka kwake hakuna hata mtu mmoja anayenufaika moja kwa moja.
Hata hivyo, Mujulizi anasema kwamba wale ambao kwa kawaida husita kuwasaidia yatima wakati mwingine huwa sahihi kwani siku hizi watu wanaendesha magari ya posh na kuishi katika nyumba za kifahari chini ya mwamvuli wa yatima. Vitendo vya aina hiyo huwakatisha tamaa watu walio tayari kuwasaidia yatima.
"Wakati mwingine, fedha wanayopewa yatima inakosa mshindo kwa vile inatapeliwa na watu wachache wasio waaminifu katika jamii," anasema akiongeza kwamba hakuna mtu atakayekuwa tayari kuwaona watu wengine wakifaidi maisha kwa pesa zilizotolewa kuwasaidia yatima wakati
watoto wao. Katika shule za kulipia visiwani wazazi wachache sana hufikiria kuwapeleka watoto wao kwenye shule za kulipia, za Msingi au Sekondari na badala yake hutegemea sana shule za umma ambazo hutoa elimu ya bure hadi ngazi ya sekondari.
Kwa bahati mbaya, shule za umma zinakosa mahitaji muhimu, kama vile madawati, vitabu vya rejea na wafanyakazi wenye uwezo.
Wakati ambapo unawekwa mkazo mdogo sana wa juhudi za kuchangisha pesa kugharimia elimu Zanzibar, familia nyingi zinatumia kiasi kikubwa cha pesa kugharimia maandalizi ya sherehe za arusi.
Michango hiyo wala haiwasaidii wanandoa wapya, bali watu wanaohudhuria tafrija.
mahitaji mbalimbali ya mavazi huongezeka, ndivyo ilivyo kwa wanawake wa Zanzibar kutaka mavazi mapya wakati wa sherehe ya arusi.
Wanawake wa Zanzibar wako nyuma sana kielimu, ikillinganishwa na wanaume, lakini ndio watumiaji wakuu wa kipato cha familia katika sherehe nyingi za arusi ambazo wanaume hawana nafasi nazo.
Lakini awali ya yote swali la msingi linabaki kuwa kwa nini wazazi, ndugu na wanaume huwekeza sana katika sherehe za arusi na wakati huohuo wakifumbia macho sekta muhimu kama vile elimu.
Ali Uki ni mwandishi wa habari wa Zanzibar na anadhani jamii inahitaji kubadilika iwapo Zanzibar inataka kuipa sekta ya elimu kipaumbele.
Watoto walio katika hali ngumu: Kwanini picha kama hii ya kusikitisha haiwagusi Watanzania wanaopenda arusi za ulimbwende
ambapo watoaji wanalazimika kujikamua ili watoe msaada.
Hata hivyo, anayapa changamoto mashirika yaliyosajiliwa au wanaojitolea wakidai kwamba yanawasaidia yatima kuwa wakweli na kujitolea kwa wito huo lakini si kuzitumia kwa kujinufaisha.
Huko Zanzibar, hivi sasa ni marufuku kuchanga pesa kwa ajili ya arusi au kuandaa sherehe ghali kwa watu ambao ndio kwanza wameoana. Hata hivyo, inapokuja kwenye kugharimia elimu, ni vigumu kuwa na mipango kama hiyo.
Wakati ambapo kupata elimu ya msingi na ya sekondari kunabaki kuwa suala muhimu kabisa, miongoni mwa wazazi Zanzibar, hapa ni vigumu familia kufikiria kufanya mpango wa kuchanga fedha kwa ajili ya kuwalipia
Kiasi kikubwa cha michango ya kifedha kwa ajili ya arusi visiwani hugharimia mavazi ya gharama kubwa kwa ajili ya wanawake wanaohudhuria sherehe na mapambo mengine, lakini ni kiasi kidogo sana kinachotumika kwa viburudisho na vinywaji.
Sherehe zinabakia kuwa miradi yenye kuleta faida kwa wanawake kununua au kuzionyesha nguo zao za gharama kubwa, wanandoa wapya au wanandoa watarajiwa wakipata faida ndogo sana ya vitu.
Tanzania Bara hali ni tofauti sana. viburudisho na pombe huchukua kiasi kikubwa cha fedha iliyochangwa kwa ajili ya sherehe ya arusi na kiasi kidogo huelekezwa kwenye ununuzi wa nguo kwa ajili ya maarusi wapya.
Kama ilivyo wakati wa siku kuu ya Noeli Tanzania Bara, wakati ambapo
Alisema kwamba kutumia fedha nyingi kwenye sherehe za ndoa, ambazo ni vigumu kudumu, ni upotevu wa rasiliamli.
Anasema sasa wakati umefika kwa wazazi wa Zanzibar kuwekeza kwa watoto wao na anasema mojawapo ya mambo ya kufikiriwa ni kutumia fedha kwa ajili ya elimu.
Bw. Uki anasema miundo-mbinu ya elimu iliyopo visiwani haitoshelezi, kwa vile kiwango cha asasi hizi za umma hakiridhishi kabisa.
Ni maoni yake kwamba mchakato halisi wa uchagiaji wa arusi ndio unaounganisha utegemeano wa kifamilia au kiunganishi miongoni mwa wanandugu wa karibu.
Huu ndio utamaduni anaosema kila mtu miongoni mwa marafiki na ndugu na kila mtu katika familia anahisi
anapaswa kufuata.
Anasema kuchepuka kutoka
kwenye kaida za desturi humweka
mchepukaji katika mgongano na jamii,
kukabiliana na vizuizi vingi licha ya
kumweka mtu katika hali mbaya na
umma.
Abdul, mfanyakazi wa hoteli kutoka
Ras Nungwi Kaskazini mwa Mkoa wa
Unguja ana mawazo kwamba umma
unapaswa kuelimishwa kutumia
sehemu kubwa ya rasilimali zake
kugharimia sekta ya elimu.
Lakini juu ya kwa nini upendeleo
uko zaidi kwenye arusi kuliko kwenye
elimu, Bw. Khamis anasema ni kwa
sababu arusi inaunganisha familia mbili
ambazo zinashindana, kila mmoja
ikitaka kuivutia nyingine.
Kila mtu kutoka upande wa familia
ya bwana arusi au bibi arusi anahisi
kwamba kuna haja ya kusherehekea
ambapo suala la elimu linahesabiwa
kuwa ndani ya familia moja yenyewe.
Anasema kuwa hakuna faida ya
moja kwa moja ya vitu kwa ndugu wa
mbali au marafiki wakati wanapotoa
mchango kwa ajili ya elimu ya mtoto
ambapo anasema unapochanga kwa
ajili ya arusi karibu unalazimika
kuhudhuria.
Anasema hii inaamaanisha kwamba
kila upande wa wenzi hawa unahisi
unawajibika kuchangia arusi kutokana
na woga tu kwamba iwapo hawatafanya
hivyo, upande mwingine utawafikiria
vibaya.
"Elimu inachukuliwa kuwa
shughuli ya mbali ya ukoo au shughuli
miongoni mwa watu wa familia
ambapo arusi inahusisha kundi kubwa
zaidi ambalo linajumuisha familia za
bwana arusi na bibi arusi zinazotoa
michango ziathirike," anasema.
Farashuu Ali Ame anasema kwamba
michango ya sherehe za arusi inatokana
na desturi ya muda mrefu ya kuamini
kwamba ndoa haiwi tu kati ya wenzi
bali ni muungano wa familia za bibi
arusi na bwana arusi.
Anasema
kwamba
kinachosherehekewa pale si ndoa ya
wenzi hao tu bali muungano wa hizo
familia mbili tofauti, ambao
unahalalisha sherehe kubwa zaidi.
Farashuu anadhani kwamba wakati
ambapo kuna haja kwa wazazi kupanga
ukusanyaji huo wa fedha uwawezesha
watoto wao kuhudhuria shule, hata
hivyo sherehe za arusi pia zidumishwe.
Khamisi Ali Shamte, mkazi wa
Kidongo Chekundu, anadhani
kwamba watu wanahisi kuwajibika
kuchangia sherehe za arusi kwa sababu
tu ya manufaa wanayoyatarajia ya
kushiriki katika hali ya usawa kwenye
sherehe yenyewe.
Anasema msukumo mkuu si
kusaidia bali kuwa sehemu ya watu
muhimu kabisa ambao wangependa
kusherehekea arusi.
JAMII NA WATOTO WALIO KATIKA HALI NGUMU
3
Watumishi
wastaafu
wawajali watoto
wa mitaani
NA JOSEPH KITHAMA
Ni jambo la kawaida kwa wastaafu wa serikali kutumia muda wao uliosalia wakihudumia biashara binafsi ili waweze kuishi kulingana na mapato, lakini watatu wao, wakiwa TemekeMtoni, Dar es salaam wana wito tofauti.
Wastaafu hao watatu wanautumia muda uliosalia kutoa elimu kwa watoto wa mitaani katika jiji na hivyo, kulilea wazo lao katika upendo mkubwa wa kuwafanya watoto wa mitaani waende shule, bila ya rasilimali zao wenyewe, hata kidogo na juu ya yote hawakuwa na jengo lolote lile la kuiendeshea shule yao.
"Mwaka 1968 tulisajili shule, kwa misingi ya hali ya utegemezi wa wafadhili ikiwa inalengwa kutoa elimu ya bure kwa watoto wa mitaani, hususan yatima, walioacha shule ya misingi na yatima wanaolazimika kuacha masomo kutokana na kutokuwa na uwezo wa kulipa ada ya shule pamoja na gharama nyinginezo," Mkurugenzi Mtendaji wa Dhamana ya Matunzo na Maendeleo ya Watoto wa Mitaani (SCCADET), Bw. Peter Nnaly
(69), lakini mstaafu, alisema.
Bw. Nnally, pamoja na Bw.Bernard
Makoja, mwalimu wa zamani ambaye
alijiunga katika siasa; na Mwalimu
Mkuu wa shule hiyo, Bi. Perpetua Nali,
hivi leo ni urithi wa kundi la
wafanyakazi wa serikali wastaafu
ambao wameshinda vishawishi vya asili
vya kushughulikia biashara zao
wenyewe ili kufuatilia kile
wanachokiona kuwa ni kusudi lenye
thamani.
"Wakati wa usiku tulianza kwa
kufuatilia sehemu za wazi ambazo
watoto wa mitaani walizitembelea
mara kwa mara, hususan wale
waliokuwa wakiuza vitu kama vile
sigara, karanga za kukaanga na maji ya
kunywa ili kuwashawishi wajiunge na
hii shule ya bure," Mkurugenzi
Mtendaji
wa
SCCADET
anakumbukia.
Kama mpango wa kuwavutia kwao,
wafanyakazi hao wa zamani wa serikali
wanalazimika kuwashawishi watoto wa
mitaani kwamba hawatapoteza biashara
ndogondogo ambazo zinawahakikishia
vipato vya kila siku kununulia walau
vitu vya msingi.
Mkutano wa Maaskofu wa Tanzania
Bw. Bernard Makoja (mwansiasa mstaafu) akimfundisha mtoto wa shule ya msingi
(TEC) uliipatia shule hiyo jengo la zamani huko Temeke Mtoni, ambalo lilikuwa likitumika kama baa ya bia. Kundi la mwanzo la wanafunzi halikuwa na madawati ya kukalia; badala yake walilazimika kusoma wakiwa wamekaa chini sakafuni.
Miaka miwili baadaye shule hiyo ilinyang'anywa jengo, jambo lililomshawishi Bw. Nnali awasiliane na ndugu zake ili watoe jengo dogo ambalo lilikuwa katika ushoroba wa mtaa wa vibandavibanda, ambavyo vilionekana kama vibanda vya kuku.
Ni Reverend Father John wa Benedictine Order ambaye aliwaunganisha na ufadhili wa Kijerumani kuhusiana na shule hiyo ambayo ilikuwa haifahamiki. Ikitumia fedha kutoka kwa mfadhili huyo, usimamizi uliibadili nyumba hiyo iliyoonekana kama banda la kuku
kuwa madarasa madogomadogo.
Hatimaye, juhudi za shule ya watoto
wa mitaani zilitambuliwa na Mfuko wa
Okoa Watoto Tanzania, ambao ulitoa
msaada wa vitu na wa kifedha kuisaidia
shule, ikiwa ni pamoja na posho ya
walimu wa kujitolea.
Mwaka 2002 juhudi za wachangiaji
wote ziliwezesha shule hiyo kuwa
miongoni mwa shule kumi za msingi
za kwanza zilizofanya vizuri katika
mitihani ya kitaifa ya Darasa la IV.
Hata hivyo, hiyo shule imeharibika
vibaya kufuatia kufungwa kwa Mfuko
wa Okoa Watoto. Watoto watatu tu
ndio waliofanikiwa kufanya mtihani
wa darala la VII mwaka 2003 kwa vile
watoto wengi walilazimika kuacha
masomo kutokana na matatizo ya
shuleni.
Shule haina maji ya bomba; milo ya
watoto
inategemea
fedha
zinazokusanywa na mwalimu mkuu kutoka kwa wanachama wenza wa Chama cha Wanawake Wakristo (WAWATA) na pamoja na waumini wengineo wa mitaani.
Dawati lililowekwa nje ya darasa linatumika kama mapokezi na meza ya chakula kwa jili ya wafanyakzi waliosalia, ambao wanatokana na wastaafu. Shule hiyo haijawahi kuwa na maji ya bomba, badala yake wanategemea maji ya mvua yanayochirizika kutoka kwenye mabati.
Hivi sasa, katika hali hiyo ya kusikitisha, shule hiyo ya watoto wa mitaani ina nafasi kumi za walimu zilizo wazi ambazo zinaweza kuendelea kuwa wazi siku zote kwa kuwa mfuko wa shule hauwezi kumudu kumlipia kila mwalimu mshahara wa Tsh. 50,000.
Watoto yatima wa `Malaika'
Onesphory, miongoni wa wajumbe wa kamati ya watoto yatima
Mtoto katika Kamati ya Yatima
Onesphory Gabriel ana umri wa miaka 13, mwanafunzi wa Shule ya Msingi Bugando.Yeye ni mjumbe wa Kamati ya MVC ya Bugando `A', akiwa Katibu wa Kamati hiyo. Onesphory anaifurahia kazi yake mpya, amepania kufanyakazi kwa bidii kama mwakilishi wa watoto wa Kata ya Bugando `A'.
Onesphory amefiwa na baba yake mwaka 1996, lakini mama yake anayefanyakazi kama Katibu Muhtasi katika Kampuni binafsi anamlea yeye na ndugu zake watatu; kaka yake mwenye umri wa miaka 16, dada yake pacha na mdogo wake wa kiume mwenye umri wa miaka 10. Wote wanaishi pamoja kama familia.
Onesphory amechaguliwa katika Kamati ya MVC wakati wa mkutano wa Hadhara wa Kata wakati mchakato wa uainishaji wa MVC ulipotambulishwa katika jamii.
Onesphory na msichana mmoja walichaguliwa kuwa wajumbe wa Kamati ya Watoto Walio Hatarini Kabisa ya Kata ya Bugando `A', wakiwakilisha sauti za yatima na watoto wengine walio hatarini kabisa.
Uteuzi wa Onesphory na mwenzake ulifanywa na Mwenyekiti wa Kata, na watoto waliohudhuria mkutano huo waliombwa maoni yao, kuwa ama waunge mkono au wakatae uteuzi wao. Watoto hao waliridhia kuwa wawe wawakilishi wao katika Kamati ya MVC.
Baadaye alichaguliwa kuwa Katibu wa Kamati. Onesphory anachukulia jukumu hilo la jamii kwa dhati kabisa. Mwishoni mwa juma hutembelea kitongoji ili kubadilishana mawazo na watoto, na kujua hali zao. Yeye ndiye aliyetupeleka kwa Hassan na Samson, baada ya kujua mateso wayapatayo nyakati za ziara zake.
NA GODFREY KALAGHO,
DAR ES SALAAM
Mfuko wa Yatima wa Malaika ndilo jina ambalo Bibi Najma Manji alilichagua kwa ajili ya makazi ili kuamsha welewa wa umma ili jamii iweze kutambua umuhimu wa kuwaokoa na kuwalinda watoto wengi wanaoishi katika mazingira ya hatari. Neno Malaika linawafananisha watoto na Malaika wa Mungu.
Yeye ni mwangalizi wa mfuko; kituo ambacho hivi sasa kinawatunza watoto 15 walio chini ya umri wa miaka 12. Mwanzoni ilikuwa nyumba ya vyumba vinne vya kulala kwa ajili yake na familia yake.
Bibi Manji alianza kuwatunza yatima wakati alipoolewa. Hisia zake kali za kuwalea yatima zilioana na zile za mumewe, ambaye mwenyewe alikua akiwa yatima.
"Tulikuwa tukiishi na yatima humuhumu, kwenye nyumba yetu. Kadiri idadi yao ilivyoongezeka ndivyo tulivyokabiliwa na upungufu wa rasiliamli, lakini ilikuwa vigumu kupata msaada kutoka jamii ya ndani na au Asasi zisizo za kiserikali. Hili likatuchochea kujitolea nyumba yetu na kuigeuza kuwa kituo cha yatima", anasema.
Kati yao hao yatima 15, wawili ni yatima wa kijamii, ambao hivi sasa wanahudhuria shule ya awali pamoja na watano wengine. Sita wako darasa la kwanza wakati mmoja yuko katika shule ya watoto wenye mtindio wa ubongo iliyoko Sinza Dar es Salaam. Mkubwa kuliko wote ana umri wa miaka 15 na hivi sasa anajifunza kushona cherahani kwenye shule ya ufundi stadi.
Kwa vile ni makazi ya familia, eneo la nyumba ni dogo sana. Wavulana wanatumia vyumba viwili, ambapo wasichana wanatumia nyumba vilivyosalia. Pia, kuna wahudumu wanne ambao wanalala ukumbini.
Nilipoingia katika kila chumba, niliona magodoro matatu au manne yamelundikwa kwenye kitanda kimoja na baadaye nilielewa kwamba yalikuwa ya wahudumu wa kike. Kila asubuhi wanapaswa waondoe mikeka yao ya kulalia na matandiko ukumbini ili sehemu hiyo iweze kutumika kama mapokezi.
"Sehemu hii ni ndogo sana, tunahitaji kuipanua, lakini hatuna fedha, "Bibi Manji alisema, akiongeza kwamba wilaya ya Kinondoni ina yatima wengi na kwamba wale walioko Malaika wana bahati kwa kuwa kituo hicho hakiwezi kuchukua zaidi.
"Idara ya Ustawi wa Jamii bado inawashauri watoto waje hapo, lakini hatuwachukui kwa kutokana na ukosefu wa nafasi," alisema.
Mchana, watoto walirejea toka shule na ulikuwa wakati wa chakula cha mchana. Watoto wengine wa mtaani walio chini ya umri wa miaka kumi, ambao wanakosa vituo vya malezi, walikuwa wamekwishafika, wakisubiri chakula.
Katika kituo hiki watoto wanaishi kama dada na kaka wa familia moja. Wanahusiana vizuri sana na watoto wa wengine ambao hawakupata nafasi, wanakula, wanacheza na kuimba pamoja.
Hata hivyo, baada ya kula, yatima wa Malaika wana ratiba ya kudumu ya shughuli nyingine na wanapaswa waondoke kwenda sehemu nyingine.
Maria Athuman, mwenye umri wa miaka 8, hana shaka kwamba Bibi Manji ndiye mama yake. Nilipomuuliza kuhusu wazazi wake, alinijibu: "Maka yangu huyu hapa," alisema akimwelezea Bibi Manji.
Ingawa kituo hicho ni safi sana, lakini Bibi Manji anawasiwasi juu ya mambo matatu. Kwanza, ni mateso ya watoto ambao bado hawajapata nafasi katika nyumba ya yatima na wanazurura mitaani wakiokoteza chakula. Anasema serikali imewapa ekari 50 huko wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani, lakini hawana pesa kuweza kuendeleza sehemu hiyo.
Pili, kituoni kuna uhaba wa maji. Ili kulijaza tanki, hawana budi kuteka maji kutoka mbali. "Kama mtoto akiugua na hakuna maji, anaweza akawaambukiza wengine kwa urahisi kabisa," anasema.
Tanki la maji lililopo lililotolewa na Shirika la Kikristo.
Tatu, Ingawa watoto hupata huduma ya tiba bila malipo kutoka hospitali za serikali, lakini gharama za tiba ni tatizo iwapo dawa zilizoandikwa hazipatikani kwa urahisi. "Inakuwa gharama kwa sababu unalazimika kwenda kwenye maduka ya dawa binafsi ambako dawa ni ghali," anasema.
Habibu Henry, mwenye umri wa miaka 12, ambaye amepooza upande mmoja, anaishi katika kituo hiki. Kwa vile hawezi kutembea bila msaada, kila mara husindikizwa shule. Aliokolewa na Chama cha Wawindaji katika Mkoa wa Iringa. Chama hicho ndicho kilichomleta Dar es salaam kwa ajili ya matibabu.
Alipoletwa kwenye Idara ya Ustawi wa Jamii, Dar es salaam, ikagunduliwa ya kwamba mtoto huyo pia alikuwa na matatizo ya akili. Hili likaifanya menejimenti ya Malaika kumtafutia shule maalumu ? kwa ajili ya watoto wenye matatizo ya ulemavu. Ilikuwa hatua isiyofaa.
Bw. Chelestino Msimbwa, Mwalimu Mkuu wa Shule Maalumu ya Sinza, ambako Habibu anasoma, ambaye mara moja aliwahi kumsindikiza mtoto huyo hospitali, alisema kwamba madaktari waligundua kwamba
Habibu anaugua ugonjwa wa "macho
kufifia" (optical atrophe). Hii ina maana ya
kwamba neva ya jicho imeathirika, na
kusababisha kuunganishwa kwa ujumbe
kutoka kwenye jicho kwenda kwenye
ubongo kwa ajili ya fasili. Alisema
anaendela vema katika masomo yake.
Bibi Betty Shija, Mwalimu mkuu wa
shule hiyo alisema kwamba Habibu haoni
vizuri "Anapata kivuli, lakini hawezi
kusoma vizuri." Idara ya Ustawi wa Jamii
walituhumu tatizo hilohilo, wakiamini
kwamba linatokana na matatizo yake ya
awali; lakini amedhihirisha kuwa wa
kawaida kabisa.
Kutokana na matatizo ya kuona
anakwepa kukutanisha nyuso na ni
mchangamfu na kama akiulizwa hupenda
kuongea juu ya mustakabali wake. Hutoa
maelezo mazuri juu ya uzoefu wake
uliopita.
"Nilizaliwa Mabalali katika mkoa wa
Iringa, nilikuwa mtoto wa kawaida Mama
yangu ni Sikamanga na baba yangu Henry
Ming'engeji. Baadaye nikatambua kwamba
siwezi kutumia mkono na mguu wangu wa
kulia. Macho yangu pia yalikuwa yanawasha
na nilipata maumivu makali. Baadaye
macho yangu yakawa dhaifu na karibu
sikuweza kudhibiti matendo yake," alisema.
Anasema madaktari wa CCBRT Dar es
Salaam
walimwambia
kwamba
wasingempasua kwa sababu ingehatarisha
maisha yake na huenda angekuwa kipofu
kabisa.
Habibu alisema kwamba aliwapoteza
wazazi wake wote wawili na akawa anaishi
na dada yake, Sipendeki. Ingawa yu salama
katika makazi ya Mfuko wa Yatima wa
Malaika, ana wasiwasi juu ya mdogo wake
wa kiume Mateso, alisema hana uhakika
kuhusu usalama wake.
"Nikikua, napenda kuwa mwalimu,
nijenge nyumba yangu mwenyewe na
kuendesha gari langu mwenyewe; anasema.
"Lakini kamwe sitaondoka Malaika,"
anasisitiza.
Anaamini kwake Malaika ni kwao, kama
ilivyo Iringa. Ari na matumaini yake
vinategemea watu wanaowalea yatima wa
Malaika.
Bibi Manji anauendesha mfuko huo
kwa msaada wa wanafunzi wake wawili wa
zamani katika shule ya msingi, ambao
aliwafundisha 1978. Wanafunzi hao ni
Hadija Membungu na Bahati Godfrey.
Majirani huwasaidia kwa ngano, sukari na
chumvi, kila wanapoombwa wasaidie.
Wamiliki wa maduka wanawakatalia
kuwakopesha
bidhaa
kila
wanapojitambulisha kama wahudumu
kutoka Mfuko wa Malaika.
4
Hali ya watoto yatima na wale wanaoishi kwenye mazingira magumu
Idadi ya watoto yatima hapa nchini ni zaidi ya milioni mbili. Yatima wanakabiliwa na mahitaji muhimu ambayo wamekuwa hawayapati kwa kiwango kinachotakiwa. Watoto wengi zaidi wamekuwa wana beba majukumu mazito yanayoshinda
umri wao: Kama vile kuwa kiongozi wa familia, kutunza wazazi wagonjwa na kufanya kazi kwa muda mrefu ili kujipatia riziki.
Mtoto anayeisha na mmoja au wazazi wake wote wakiwa wagonjwa, hushindwa kwenda shule, kwa
kuwa lazima atafute pesa kwa kufanya kazi za ziada ikiwa ni pamoja na kulima.
Ingawa mtoto huyo si yatima, lakini atakosa haki zake nyingi za msingi na atajikuta katika hatari ya kunyonywa na kudhalilishwa.
Habari zote na UNICEF Tanzania
Kina bibi ndiyo walezi wakubwa wa yatima Tanzania
Eliza Kulola, ana umri wa miaka 68, na ni mjane. Akiwa amekaa katika mkeka nje ya kibanda kilichoezekwa nyasi na kuku wakila, Eliza anazungumzia mzigo wa kulea wajukuu watano akiwa peke yake.
Wajukuu wa Eliza wana umri wa
miaka 16,15,13,7 na 4. Anaishi nao wote
katika kijiji cha Nyagusa, tangu wafiwe na
mama zao. Anaonekana amechoka na
kukosa matumaini wakati akizungumzia
maisha yake na familia aliyonayo hivi sasa.
Kwa sasa wasiwasi wake ni hatima ya
watoto," Kusema kweli, sifikirii namna ya
kuwalisha wajukuu zangu, kwa sababu
kutoka shamba langu dogo na misaada ya
jirani tunaishi. Wasiwasi wangu zaidi ni
majaaliwa yao baada ya mimi kufariki,
mimi ni mzee na hushambuliwa na
malaria mara kwa mara, Sijui!," alisema
Eliza huku akiwa amekaa mkekani akiwa
na kitukuu chake cha umri wa miezi 8 Eliza Kulola (miaka68 ) akiwa na wajukuu (kutoka kushoto) Neema
magotini.
(miaka 13), akiwa amapakata Moses (miezi 8), Noel (miaka4) na
Kwa miaka 7 iliyopita Eliza amekuwa Zacharia (miaka7)
akiwauguza mabinti zake watatu mmoja baada ya mwingine, mpaka walipokufa na kuwaacha watoto 5. Mpaka
sasa Eliza anategemea zaidi kilimo cha kawaida kujipatia riziki. Analima mhogo na mtama karibu ya nyumba yake,
kiasi cha kujipatia chakula, aidha anauza kuni kufidia mahitaji ya kaya. Hajawahi kusoma na mpaka sasa hawezi
kusoma wala kuandika.
Miongoni mwa wajukuu zake ?Emma 7, Jennifer 9 na Neema 13, ndio wapenzi wake, kwa sababu wanasaidia
kazi za nyumbani. Wasichana hao wanakata kuni kwa ajili ya kupikia na kuuza, kuteka maji, kumtunza mtoto wa
miaka 4. Bila shaka, kazi zote za nyumabni zinawaangalia wao. Ingawa wanasoma, hawana muda wa kujisomea
nyumbani au kufurahia utoto wao.
Neema, 13, anajua machache kuhusu baba yao. anajua kuwa ni askari. Hajafika kuwaangalia, tangu mama yao
afariki dunia miaka 5 iliyopita. Neema anapenda shule, na anahakikisha kuwa anaweza kununua madaftari yake ya
shule kwa kuuza kuni. Bei ya mzigo mmoja wa kuni ni sh. 200 (sawa na robo dola ? senti 20).
Bibi Eliza anaonekana amechoka, ndio anapata nafuu ya malaria, na ana wasiwasi kuwa mbu watawang'ata
wajukuu wake. Wanalala pamoja katika chumba kimoja, hawatumii chandarua kwa sababu hawana uwezo wa
kununua.
Watoto kama Watunzaji Wazazi Wagonjwa
Katika umri mdogo sana,Veronika Simon tayari ni mtu mwenye majukumu ya familia na kumtunza mama yake mgonjwa. Msichana huyo ana umri wa miaka 13 na mwanafunzi wa Shule ya Msingi Nundu. Veronika anaishi na
mama yake Lucia Ganzia aliyefikisha umri wa miaka 50, ingawa
anaonekana kama ajuza wa miaka 70. Hapana shaka, UKIMWI
umedhoofisha mfumo wake wa kinga na kukondesha mwili wake.
Anazungumza na kutembea kwa taabu sana, na akipata nguvu ya
kusema utaona hisia ya maumivu usoni mwake.
Lucia anaishi na mjukuu wake Yohana Simon mwenye umri wa
miaka 11. Yohana anasoma pamoja na Veronica. Lucia anategemea
sana ukoo wake mpana na wasamaria wema kuwalisha na kuwavalisha
watoto wake, na kadiri anavyozidi kuugua na kudhoofika, msaada wa
familia unazidi kupungua na anategemea zaidi Kituo cha UKIMWI
cha jamii.
Hata siku tulipowatembelea, Veronica alikuwa amemsindikiza
mama yake katika Kituo cha Mapumziko cha UKIMWI cha
MWAOMI, kuchukua dawa na chakula. Kituo hicho kinamilikiwa na
Kanisa la Anglikana, kikitoa msaada wa wastani kwa watu
wanaoathiriwa na VVU/UKIMWI.
Veronica Simon anamuuguza mama yake
Lucia anajiona mjane, kwa sababu tangu mwaka 1997 hajawasiliana aliye taabani
na mume wake, baba wa watoto wake.
Lucia ameonekana na virusi vya UKIMWI mwaka 1997, na ana uhakika kuwa ameambukizwa na mume wake,
aliyekuwa akiumwa mara kwa mara lakini alikataa kukubali au kwenda kupimwa. Alianza kuumwa mwaka 1998,
aliumwa kiasi cha majirani kumpeleka hospitali na kulazwa katika wadi ya wagonjwa wa TB. Mtoto wake wa kiume
ambaye wakati ule alikuwa na umri wa miaka 11 ndiye aliyekuwa mlezi mkuu; kupika na kupeleka chakula
hospitali.
Kwa miaka yote, Lucia amekuwa akilazwa na kutolewa hospitali kwa maradhi mbalimbali na maambukizo
nyemelezi, na Veronica ndiye pekee anayehudumia mahitaji yake. Ana wasiwasi kwamba mtoto wake wa kiume
mara nyingi hayupo nyumbani kwa sababu amechoka kumhudumia.
Veronica yuko darasa la 5 lakini mahudhurio yake yamekuwa mabaya; wakati mwingine haendi shule kwa
majuma kadhaa, kwa vile anakaa nyumbani kumhudumia mama yake mgonjwa. Familia inamtegemea Veronica
kutafuta fedha. Msichana huyo anapika maandazi anayouza duka la jirani. Wakati mwingine Lucia anapojisikia
ahueni, anamsaidia binti yake kukanda maandazi.
Kadiri afya ya Lucia inavyozidi kuwa mbaya, hakuna hata mmoja katika ukoo mpana aliyejitokeza kuzungumza
naye kuhusu majaaliwa ya watoto wawili. Kwa Lucia ina maana kuwa hakuna hata mmoja anayetaka kuchukua
jukumu la kulea watoto, na hili linamvunja moyo, kwa kufikiri wataishije baada ya yeye kufariki dunia!
Familia zabebeshwa mzigo mzito
Kata ya Bugando Mission, Mwanza. Samson ana umri wa miaka 8, Hassan 10 na Rahel Khalfan 14 na wote ni yatima, waliofiwa na wazazi wao miaka mingi iliyopita. Rahel na Hasaan angalau wanakumbukumbu za baba yao, kuwa mkulima aliyemiliki shamba kubwa. Hawakumbuki kijiji walichokuwa wakiishi, ila tu ilikuwa Mkoa wa
Uporaji wa urithi wa watoto
Juma Joseph, umri wa miaka 15, alikuwa darasa la 5 katika Shule ya Msingi Bungarika kabla ya kuacha shule. Hivi sasa anazurura, akipitisha muda wake vijiweni.
Juma ameacha shule kwa sababu alirudishwa nyumbani na waalimu kwa kukosa sare za shule. Alipomwambia
mjomba wake, alikataa kumnunulia sare na kumlazimisha arudi shule akawaambie walimu kuwa "hakuna mtu wa
kununua sare" Mtoto alikataa kurudi kwa kuogopa kuaibishwa na hivyo kuamua kubaki nyumbani.
Mjomba wao aliamua kuwachukua baada ya baba yao kufariki, amekuwa akimtesa Juma na mdogo wake.
Mara nyingi juma anafokewa na kujenga chuki kati yake na mjomba wake. Amekuwa akimwambia Juma kuwa
hawezi kuendelea kumlisha yeye na mdogo wake Emmanuel mwenye umri wa miaka 12.
Juma na Emmanuel ni yatima, wamefiwa na wazazi wao wote tangu mwaka 1999 na 2000; Baba yao alitangulia
kufariki dunia, halafu akafuatia mama yao. Hawajui kilichowaua wazazi wao, lakini wanakumbuka tu kwamba wote
walikuwa nyondenyonde kila siku, na walikuwa wakienda hospitali mara kwa mara.Wala hakuna hata mtu mmoja
aliyewaambia kilichokuwa kikiwasumbua.
Baba yake Juma ana nyumba walioozoea kuishi kama familia. Baada ya kifo cha mama yao, Juma na Emmanuel
walihamishiwa kijijini kuishi na shangazi zao. Maisha yalikuwa magumu kijijini kwa sababu shule ilikuwa mbali
na watoto walikuwa wamechanganyikiwa. "Kaka yao mkubwa aliamua kuwarudisha mjini, na kujiunga tena na
shule yao ya zamani.
Watoto walipata pigo la pili wakati kaka yao mkubwa alipougua na baada ya kwenda hospitali akapimwa na
kugunduliwa ana T.B. Alidhoofika haraka na kufariki mwaka 2004.
Walihamishiwa kwa ndugu mwingine, mjomba, wanakoishi hivi sasa. Mjomba wao anayewalea ndiye pia
mdhamini wa nyumba yao ya familia. Ameikodisha nyumba hiyo, anakusanya kodi kila mwezi na kutumia fedha
hizo kwa matumizi yake ya binafsi.
Amewaambia watoto hao kuwa fedha ya pango anayokusanya ndiyo wanayotumia katika familia kwa chakula
na mahitaji mengine
madogo madogo.
Juma
na
Emmanuel wanajua
wazi
kwamba
anachofanya mjomba
wao si haki, lakini
ndugu zao wote
wamenyamaza.
Wanajaribu kuomba
msaada kutoka kwa
viongozi wa kijiji,
lakini mlolongo ni
mrefu na wa polepole
mno! Juma bado
haendi shule na
haielekei
kama
atarudia shule yake
hivi karibuni!
Juma (miaka 15) na Emmanuel (mika 12) wameporwa nyumba yao na mjomba
Kigoma. Rahel
anakumbuka kuwa
ilikuwa upande gari
la moshi ili ufike
kijijini kwao.
Watoto hao hivi
sasa wanaishi na
Ashura Chishako,
ambaye ni dada wa
marehemu mama
yao. Ashura ni mjane
Mama mmoja anayeishi Wilayani Makete akiwa na wanae pamoja na watoto yatima wa ndugu zake
baada ya mume wake kumtelekeza na watoto 8. Ashura
hajasoma, yeye ni mchuuzi wa ndizi na anajipatia Tsh. 500 kwa siku (sawa na nusu dola) na kulisha familia ya watu
12.
Watoto wamechanganyikiwa, wamevaa matambara (nguo mbovu), wana njaa na Hassan alikuwa analia.
Wavulana wawili wanasoma shule ya msingi Bugarika, lakini msichana anabaki nyumbani kusaidia kazi zisizo na
kikomo na kuuza ndizi. Samson ni mzungumzaji sana, na anaeleza haraka maisha yao na shangazi yao Ashura mjini
Mwanza.
Sentensi ya kwanza ya Samson ni kwamba wanakula mara moja kwa siku wakati mwingine hata huo mlo mmoja
unakosekana. Kwa kuwa ilikuwa mwezi mtukufu wa Ramadhani msimu wa waislamu kufunga saumu Samson
husema kuwa "Ni afadhali tufunge saumu, kwa sababu hatuli chochote mchana."
Samson na kaka yake hawana chumba katika nyumba ya familia, kwa sababu kitanda kimoja analalia shangazi
yao na baadhi ya watoto wadogo na wasichana wakubwa wanalala ukumbini. Wavulana wanalala stoo, kunakolala
kuku na mabata. Wanalala chini kwa kujifunika magunia ya zamani. Mahali hapo ni pabaya sana! Samsoni amesema
kuwa usiku mifugo inawasumbua kwa kuwanyia usoni, mikononi na miguuni.
Shangazi yao huwatukana na kuwapiga kiasi cha kuwaudhi. Ili kuongezea mapato ya familia, wavulana na dada
yao lazima wafanyekazi sana. Wavulana wamejenga tabia ya kufanya kazi kila siku ya kuokota mkaa katika jaa la jiji
kwa matumizi ya nyumbani kila wanaporudi shule. Wakati mwingine wanapokosa mkaa wa kutosha, shangazi yao
huwapiga na kulala bila ya chakula.
Samson anaonekana kuwa mzigo na mtundu zaidi. Siku moja Ashura alimpa Samson Tsh. 200 akanunue nyanya,
lakini alinunua za Tsh. 100 tu na kutumia 100 nyingine kununulia maandazi. Shangazi alikasirika na kumpiga sana
mpaka majirani wakaingilia kati. Tukio hilo la unyanyasaji limeripotiwa Polisi, walimwomba shangazi ajaribu
kuwatendea ubinadamu watoto hao. Tabia ya Samson inamkasirisha sana Shangazi yake.
Ni dhahiri kwamba mzigo wa kuwa mkuu wa kaya kubwa kama hiyo ni mzito mno kwa mama mjane kama
Ashura. Mfumo wa ukoo mpana ulitumika kuwalea yatima kutoka ndugu zao unakuwa mzigo mzito!
Kwa maoni: Andika Kitengo cha Mawasiliano UNICEF Tanzania P.O. Box 4076 Dar es Salaam, Barua pepe: daressalaam@ Kwa habari zaidi soma:
................
................
In order to avoid copyright disputes, this page is only a partial summary.
To fulfill the demand for quickly locating and searching documents.
It is intelligent file search solution for home and business.
Related download
- jamhuri ya muungano wa tanzania taasisi ya kuzuia na kupambana pccb
- kodi na ushuru mbalimbali 2019 2020 tanzania revenue authority
- utangulizi kwa elimu ya kifedha maelezo sahihi
- w ripoti fupi ya nchi kuhusu kazi zenye staha tanzania bara
- ushawishi wa bajeti ya afya katika serikali ya tanzania
- mwongozo wa uendeshaji vikundi vya wapanda miti wa tanzania
- ujana salama muundo wa ziada ya pesa cash plus kuhusu ustawi na
- uboreshaji wa mazingira wezeshi ili kuongeza ushiriki wa vijana esrf
- utangulizi ni wakati wa uchumi biashara na ujasiriamali kila mwaka
- printed in tanzania 2014 get value
Related searches
- po box 2005 greenville tx
- 2005 events timeline
- 2005 events in america
- year 2005 events timeline
- 2005 f150 5 4 engine diagram
- major events 2005 2015
- major events from 2005 to present
- 2005 major events in america
- important events in 2005 in usa
- 2005 ford 4 6 engine specs
- historical events in 2005 2010
- significant events 2005 present